Sunday, April 1, 2012

NADIR HAROUB ALISTAHILI JANA KUCHEZA AU LA ?



Kanuni  YA 25 ya udhibiti wa wachezaji :
Tff itadhibiti mienendo ya wachezaji kwa kuchukua hatua kama ifuatavyo.

A) MCHEZAJI ATAKAYETOLEWA NJE KWA KADI NYEKUNDU BAADA YA KUPATA KADI MBILI ZA NJANO, HATARUHUSIWA KUCHEZA MCHEZO MMOJA
B) MCHEZAJI ATAKAYEPEWA KADI NYEKUNDU ( STRAIGHT RED CARD ) ATAKOSA MICHEZO MIWILI. 
C) MCHEZAJI ATAKAYETOLEWA NJE KWA KADI NYEKUNDU KWA KOSA LA KUPIGA AU KUPIGANA ATASIMAMA KUSHIRIKI MICHEZO MITATU INAYOFUATA YA KLABU YAKE NA ATALIPA FAINI YA TSH 500,000
D) WACHEZAJI 5 WAKIPATA KADI KTK MCHEZO MMOJA KLABU ITALIPA FAINI  YA TSH 500,000
E) MCHEZAJI AKIPATA KADI JUMLA YA KADI TATU ZA NJANO ATASIMAMA MCHEZO MMOJA

PATRICK MAFISANGO IS BACK IN THE BUSINESS !

KIUNGO WA KIMATAIFA WA RWANDA MWENYE ASILI YA CONGO DRC MUTESA PATRICK MAFISANGO AMERUDISHWA KUNDINI KWA AJILI YA SAFARI YA ALGERIA,
KIUNGO HUYO ALIYEKUA AMESIMAMISHWA NA KLABU YAKE YA SIMBA AMERUDUSHWA KIKOSINI BAADA YA KUTAMBUA KOSA LAKE NA KUOMBA RADHI KWA MWALIMU,WACHEZAJI NA VIONGOZI.

Utoaji tuzo za EJAT kwa Waandishi Bora wa Habari Tanzania


 Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti (SBL) Teddy Mapunda akikabidhi tuzo kwa mwandhishi wa habari wa Mlimani Radio Tuma Dandi mshindi wa habari za watu wenye ulemavu- Redio
 Rais Dkt. Jakaya Kiwete akimkabidhi tuzo Mshindi wa Jumla wa tuzo za Mwaka huu za EJAT, Nevile Meena ambayo ilienda sambamba na Hundi ya USD 4000.
 Fili Karashani akipokea tuzo kutoka kwa Rais Jakaya Kiwete na Hundi ya Sh Milioni 10.
 Mkurugenzi wa Executive Solution, Agrey Mareale (kushoto) akikabidhi tuzo, Cheti na zawadi ya Laptop, Mshindi wa tuzo ya Mpigapicha Bora, Hamis Hamad "Mkojani"  kutoka Magazeti ya Chama cha Mapinduzi.
 Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF) Ernest Sugura (kulia) nae akikabidhi moja ya tuzo hizo.
 Mwakilishi wa TBC Dodoma, Victoria nae alipokea tuzo yake.
 Rais Dkt. Jakaya Kiwete akizungumza jambo na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginal Mengi wakati walipokutana katika halfa hiyo ya utoaji tuzo za EJAT.
Muhidin Michuzi ambaye ni mpigapicha wa siku nyingi nchini akimpongeza Hamisi Hamad kwa kutwaa tuzo ya Mpigapicha Bora.

Elfu 55 ya Wema yakataliwa na Diamond amwaga Chozi ukumbini.


 Marafiki wa Wema Sepetu wakijaribu kumbembeleza wakati akimwaga chozi... huku watu wengine wakishangilia na kuimba aibu yetu au aibu yao???
 ...hapa mwanadada akijaribu kubembeleza bila matumaini.
 Msanii wa kizazi kipya, Ommy Dimpozzz akimpa sapoti Diamond...huku akitoa ushuhuda wa maisha yake na    ya Diamond walipotoka.
 ...baada ya ujumbe wa Ommy Dimpozz, Diamond alimwaga chozi na hapa 
 alikuwa akijifuta. Picha zaidi ingia http://kajunason.blogspot.com/

SEMINA YA MAWAKALA WA MISS TANZANIA 2012 YAKAMILIKA


 Wakala wa Miss Tanzania 2012, kutoka Ukonga jijini Dar es Salaam, Daudi Mambya akichangia mada wakati wa semina ya siku mbili ya Mawakala wa Redds Miss Tanzania 2012 iliyofanyika kwa siku mbili na kumalizika tarehe 29.03.201 jijini Dar es Salaam.
 Katibu wa Kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majalkiwa (kulia) akizungumza wakati wa Semina ya Mawakala wa Mashindano ya Redds Miss Tanzania 2012 inayofanyika kwa siku mbili na kumaliza jana jijini Dar es Salaam. Pamoja nae ni  Mkurugenzi wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashim Lundenga.
 Wakala wa Miss Tanzania 2012, kutoka Mara, Godsos Mkama akichangia mada wakati wa semina ya siku mbili ya Mawakala wa Redds Miss Tanzania 2012 iliyofanyika kwa siku mbili na kumalizika tarehe 29.03.2012 jijini Dar es Salaam.
 Wakala wa Miss Tanzania 2012 kutoka Mkoa wa Shinyanga, Asela Magaka akichangia mada wakati wa semina ya siku mbili ya Mawakala wa Redds Miss Tanzania 2012 iliyofanyika kwa siku mbili  jijini Dar es Salaam.
Washiriki mbalimbali ambao ni Mawakala wa Miss Tanzania wakifuatilia mada mbalimbali katika semina hiyo .

Tuesday, March 20, 2012

Basi la Prince Muro lapata ajali Usiku wa kuamkia Leo Tunduma

Basi la Kampuni ya Prince Muro lenye namba za usajili T 485 BQV lililokuwa likifanya safari yake ya kutoka Dar es Salaam kuelekea Tunduma mkoani Mbeya limepoata ajali na kupinduka usiku wa kuamkia leo.

Ajali hiyo iliyotokea wakati dereva wa basi hilo akijaribu kulipita Lori katika maeneo ya Senjele wakati likielekea Tunduma na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 14.

Hivi ndivyo zinavyo onekana Damu na viti kuharibika vibaya baada ya ajali hiyo iliyo tokea jana usiku

Baadhi ya mabaki ya vitu baada ya ajali hiyo jana usiku

Hili Ndilo Gari la mizigo ambalo basi la Price muro lilitaka kulipita, na  baadae kushindwa na kupinduka baada ya kukutana na Gari lengine mbele yake


Shimo hili limechimbika wakati wa ajali hiyo ilipo tokea jana usiku.
Picha zaidi  MBEYA YETU BLOG

Lowasa , Mwinyi waongoza sherehe za kuzaliwa jimbo jipya la Kanisa Katoliki Ifakara


Mh. Lowassa akiwapungia mkono wakazi wa Ifakara wakati alipohudhuria sherehe za uzinduzi wa Jimbo jipya la Kanisa Katoliki Ifakara.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera wakati alipokuwa akiwasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero,kabla ya safari ya kuelekea kwenye Sherehe ya Kuzinduliwa kwa Jimbo Jipya la Kanisa Katoliki Ifakara na kusimikwa kwa Askofu Mpya wa Jimbo hilo.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akiongozana na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Mh. Joel Bendera wakati wakielekea kwenye Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilombero leo.Watatu Kulia ni Mke wa Waziri Mkuu Mstaafu,Mama Regina Lowassa.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili,Mh. Ally Hassan Mwinyi (kushoto) na Mkewe Mama Sitti Mwinyi (katikati) wakiwa kwenye mazungumzo na Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa (wa pili kulia) pamoja na Mkewe Mama Regina Lowassa (kulia) kabla ya kuanza safari ya kuelekea kwenye Sherehe ya Kuzinduliwa kwa Jimbo Jipya la Kanisa Katoliki Ifakara na kusimikwa kwa Askofu Mpya wa Jimbo hilo,Muhashamu Salitaris Melchior Libena iliyofanyika leo Ifakara,Wilayani Kilombero Mkoani Morogoro.
Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowasa akisalimiana na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dk. Hadji Mponda kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Joel Bendera na Mzee Alli Hassan Mwinyi.
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili,Mh. Ally Hassan Mwinyi akihutubia kwenye Sherehe hizo.
Mh. Lowassa akibadirishana mawazo na Askofu Mkuu wa Jimbo la Songea.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akisalimiana na Muadhama Polycarp Kardinali Pengo mara baada ya kumalizika kwa Sherehe ya Kuzindua Jimbo Jipya la Kanisa Katoliki Ifakara na kusimikwa kwa Askofu Mpya wa Jimbo hilo iliyofanyika leo Ifakara,Mkoani Morogoro.
Mh. Lowassa akizungumza na Mmoja wa wananchi wa Mji wa Ifakara.
Waziri Mkuu Mstaafu,Mh. Edward Lowassa akitoa salamu kwa wakristo waliofika kwenye Sherehe hizo leo,ambapo ameliomba Kanisa Katoliki kuisaidia serikali katika kukabiliana na tatizo la ajira kwa vijana.
Askofu Mkuu Mpya wa Jimbo la Ifakara,Muhashamu Salitaris Melchior Libena akiongoza ibada yake ya kwanza akiwa ni Askofu wa Jimbo Jipya la Ifakara mara baada ya kusimikwa leo.
Askofu Mkuu Mpya wa Jimbo la Ifakara,Muhashamu Salitaris Melchior Libena akitoa baraka zake kwa Viongozi wa Serikali waliohudhulia Sherehe hizo za kusimikwa kwake leo.
Waumini wa Kanisa Katoliki Ifakara wakiwa katika ibada hiyo.
Kwaya ya Watoto ikiimba katika ibada hiyo.