Wednesday, April 13, 2011

DINNER YA JUBILEE YA MIAKA 25 YA NDOA YA BW NA BIBI MSAFIRI ILIYOFANYIKA JUMAMOSI YA TAREHE 09.04.2011 KWENYE HOTELI YA COLLUBUS-KIJITONYAMA

 Bw na bibi msafiri mara baada ya kuwasili katika ukumbi wa hoteli ya collubus.
 Bw  na bibi msafiri wakipata kilaji.
 Bw msafiri akiwa anatafakari jambo.
 Bi Zena  akiwa kwenye pozi la jubilee
 Bw na bibi Msafiri wakiwa ya jubilee.
 Mwaaa hii ndiyo staili ya jubilee.
 Mzee Chabanga Hassani Dyamwale akitoa neno la jubilee.


 `Wageni waalikwa Brenda kushoto Eveta kati na Maria kulia
 Bw na bibi Faraji wa E.A.D. wakiwa miongoni mwa wageni waalikwa.
 Mkufu akiwa ndani ya jubilee.
 Wageni waalikwa wakiwa wanapata kitu roho inapenda.
 MC Kim Kimenya akihosti mnuso.
Mariam kulia na Brenda kushoto wakitawala mchezo.

Monday, April 11, 2011

MAFUNZO YA KAMPENI DHIDI YA MAGONJWA YASIYOPEWA UMUHIMU YAANZA BAGAMOYO

 Mkufunzi wa mafunzo yaliyofanyika katika kituo cha shule ya msingi Mwambao ya mjini Bagamoyo kushoto Bw.karindima kutoka idara ya afya ya Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo akiwa na mwenyekiti wa mafunzo kulia wakifuatilia mafunzo siku ya Alhamisi tarehe7,Aprili,2011.
 Washiriki wa mafunzo wakifuatilia mafunzo.Washiriki wa mafunzo hayo walikuwa watumishi kutoka idara za afya na elimu kwa ngazi za vijiji vya Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo.
 Washiriki wa mafunzo wakati wa mapumzilko
Mkufunzi wa mafunzo Bibi Agness Manyama kutoka idara ya afya ya Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo akifafanua jambo kwa washiriki wakati  mafunzo hayo.Kwa mujibu wa taarifa ya Manyama kampeni hiyo itaanza kati ya mwezi Aprili na Mei 2011 baada ya mafunzo ya makundi mengine yatakayohusika katika kampeni kufanyika.

Thursday, March 31, 2011

MASHUJAA MUSICA KUKAMUA KIJIJI CHA MAKUMBUSHO

Kiongozi wa bendi ya Mashujaa Musica Edward Antony a.k.a Jado F.F.U akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es salaam jana kuhusu onesho lao linalotarajiwa kufanyika kijiji cha Makumbuso siku ya Aprili mosi 2011,na kusindikizwa na Mapacha watatu.Kati ni meneja wa bendi Mujibu na kulia kabisa ni Yanick Sauti ya radi.

Saturday, March 26, 2011

KASHESHE KUELEKEA KWA BABU

Abiria wa basi la kukodi kutoka wilayani Nzega wakisukuma gari lililokwama kwenye mpaka wa Serengeti na Loliondo siku ya Jumatano iliyopita kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katIka maeneo hayo.Hii ni safari ya kuelekea kijiji cha Samunge kwa mchungaji Ambilikile Mwasupile kwa ajili ya kupata kikombe.

Friday, March 25, 2011

MKAPA AOMBOLEZA WAJAPANI

Rais mstaafu wa Tanzania Bw.Benjamin Mkapa akipeana mkono na balozi wa Japani nchini leo asubuhi alipokwenda kwa maombolezo ya wajapani waliyokosa makazi na waliyokufa kutokana na maafa ya tsunami yaliyotokea majuma mawili yaliyopita.

Saturday, March 19, 2011

KIMKEV ENTERTAINMENT KUTOANDAA MISS TANZANIA KANDA YA MASHARIKI 2011

Kwa masikitiko makubwa nasikitika kuwataarifu kuwa hatutoandaa na kuratibu mashindano ya Miss Tanzania kanda ya Mashariki 2011 kutokana na kuzidiwa na majukumu mbalimbali.

Taarifa hii inahusu pia kutoandaa  na kutoratibu mashindano ya ngazi yoyote ya Miss Tanzania kwa kipindi cha mwaka 2011.

Tunatambua kutowafurahisha mashabiki na wenye mapenzi mema nasi wanaotambua uwezo wetu wa kupanga na kusimamia matukio kwa maamuzi haya.

Tunatoa shukurani zetu kwa wote waliotuunga mkono kwa kipindi chote hasa kamati ya Miss Tanzania, waandaaji wa mikoa na wilaya ndani ya kanda ya Mashariki,warembo,wasanii,wadhamini (Vodacom,Redds Hillside Bagamoyo, Clouds redio,blog ya Michuzi,blog ya Michuzijr,blog ya OthmaniMichuzi,City style hotel,na Lindi oceanic hotel),Marafiki wetu(Albert Kawogo wa Free voice Investment Company Ltd,Mbunge wa Bagamoyo Dr.Shukuru kawambwa na wengi ambao ni vigumu kuwataja kwa sasa.

Kimkev Entretainment bado ni mwana familia ya Miss Tanzania.Tunawatakia maandalizi mema waandaji wa taifa na waandaaji wa ngazi zote kwa mwaka 2011,tupo pamoja nanyi kwa ushauri na mengine yote yatakayokuwa ndani ya uwezo wetu.


Kim H.J.Kimenya
Mkurugenzi

02Januari,2011

Sunday, January 2, 2011

KUMBUKUMBU YA DINNER YA KUWAAGA WAREMBO WA KANDA YA MASHARIKI ILIYOFANYIKA KWENYE HOTEL YA CITY STYLE SINZA AGOSTI 2010

 Mkurugenzi kim kimenya akimkadhi posho ya kujikimu mrembo Angelina Ndege posho ya kujikimu kwa ajili ya kambi ya Miss Tanzania
Wadau wakijumuika kwa pamoja kuwaaga warembo wa kanda ya mashariki kabla ya kujiunga na kambi ya Miss Tanzania 2010