Tuesday, September 20, 2011

SERENA ATOZWA FAINI KWA KUTUKANA



Serena Williams ametozwa faini ya dola 2,000 na ameepuka kufungiwa mashindano makubwa baada ya kumtolea maneno makali mwamuzi Eva Asderaki katika fainali ya US Open.

Sam Stosur alishinda mchezo huo kwa 6-2 6-3 baada ya Williams kuambiwa amekiuka taratibu kwa kutoa kauli za utovu wa nidhamu.

Williams alikuwa anatumikia muda wa miaka miwili wa kuchunguzwa tabia yake kutokana na kitendo kama hicho alichofanya mwaka 2009.

Tukio hilo lilitokea wakati Williams alipoonekana amefanikiwa kupata ponti lakini neno alilotumia kwa kupaza sauti la "Come on!" akionesha hasira fulani, lilitafsiriwa kwamba alilitoa kabla ya Stosur hajapata nafasi ya kuurejesha mpira kwake.

Pointi na mchezo katika seti ya pili alipewa Stosur na akiwa amekasirika Williams akamtolea maneno makali mwamuzi kutoka Ugiriki Asderaki.

Williams, mwenye umri wa miaka 29, alipewa hundi ya dola milioni 1.4 baada ya kuwa mshindi wa pili.

No comments:

Post a Comment