Thursday, August 29, 2013

MWENGE WA UHURU 2013 WAZINDUA MIRADI BAGAMOYO


Kiongozi mbio za Mwenge ahimiza umoja na mshikamano
Na bloger team,Bagamoyo.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa, Juma Ally Simai amewahimiza watanzania kuwapuuza watu wanaotaka kuwatenga wananchi kwa itikadi za kidini au za kisiasa na kusema kuwa watu hao sio wema kwa sababu wanataka kuingiza nchi kwenye machafuko kwa ajili ya maslahi yao binafsi.

Kiongozi huyo wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amesema hayo leo wakati wa kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa mkuu wa mkoa wa Pwani, Mwantumu Maiza aliyepokea Mwenge huo kutokea mkoa wa Morogoro.
Simai aliyasema hayo kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara wilayani hapa alipozindua miradi ya madarasa mawili ya shule ya sekondari Bwawani,Nyumba ya mganga wa  Zahanati ya Ubena Zamozi zote za Kata ya Ubena, Kituo cha Upimaji na ushahuri nasahaĆ .

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya bagamoyo.  Ahmed Kipozi alisisitiza ushirikiano na kureta tija kwa wilaya kwa kuwataka wananchi kulinda miradi inayozinduliwa na mwenge huo.

mwenge huo pia ulizindua miradi mbalimbali ikiwemo yaWodi ya wazazi kituo cha afya chalinze,jengo la madarasa 2 sekondari ya Mboga,kuweka jiwe la msingi ofisi ya kata msata na miradi mingine mingi.
Aidha Mwenge huo kesho unatarajiwa kukabidhiwa Wilayani Kibaha. na pwani unakuwa mkoa wa 23 kupitiwa na mwenge huu

Mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Maiza akipokea Mwenge wa Uhuru 2013. ..ulipoingia Bagamoyo kutokea Morogoro asubuhi ya Agost 29.