Thursday, October 2, 2014

Timu ya mpira wa pete Ikulu yawapa kichapo Ukaguzi


  Wachezaji wa timu ya mpira wa pete ya Ikulu wakiwa wamejipanga tayari kuanza mechi yao dhidi ya timu ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali uliochezwa jana uwanja wa Jamhuri Morogoro.

Mchezaji wa timu ya Ikulu Monica Kassy akiwa katika harakati za kuwania mpira katika mechi yao dhidi ya Ukaguzi jana katika uwanja wa Jamhuri Morogoro.


              Baadhi   viongozi wa benchi la ufundi la timu ya Ikulu.



Baadhi ya wanamichezo wa timu ya Ikulu wakiishangilia na wakishudia timu yao ikiwasasambua vilivyo timu ya  ya Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa kuwafunga magoli 48 kwa 13 jana mjini Morogoro.
 

(Picha zote na Eleuteri Mangi –MAELEZO



Na Eleuteri Mangi –MAELEZO

01/10/2014

Timu ya mpira wa pete ya Ikulu imeendeleza kichapo kwa timu pinzani inyokutana nazo katika mashindano ya SHIMIWI yanayoendelea mjini Morogoro.

Ikiwa imekamilika katika idara zote, timu ya Ikulu imetakata vilivyo kwa kuwafunga Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali kwa magoli 48 kwa 13.

Ushindi huo umekuja baada ya safu ushambuliaji kutekeleza wajibu wao vilivyo wakiongozwa na Monica Kassy anayechezea nafasi ya (GS) wakati nafasi (GA) amecheza Irene Elias na nafasi ya (WA) Mwadawa Twalibu ameitendea haki ambapo timu yake imefanikiwa kuibuka kwa ushindi huo mnono.

Kiungo mchezeshaji wa timu ya Ikulu Sophia Komba (C) aliipanga vilivyo timu yake na kuhakikisha timu inaelewana na klucheza kwa umahiri mkubwa mbele ya wapinzani wao timu ya Ukaguzi ambao hawakufurukuta vipindi vyote viwili vya mchezo ambapo kipindi cha kwanza hadi mapumziko Ikulu walikuwa wanaongoza kwa magoli 25 kwa 05 dhidi ya Ukaguzi.

Safu kamili inayounda kikosi cha mpira wa pete kinawajumuisha wachezaji saba na wawili wakiwa wachezaji wa akiba.

Wacheazji hao ni Monica Kassy (GS), Irene Elias (GA), Mwadawa Twalibu (WA), Sophia Komba (C), Paskalia Kibayasa (WD), Lilian Syilidion (GD) na Tatu Kalembo (GK).

Wachezaji wengine wa akiba katika mchezo huo walikuwa Jenifer Mwandupe na Nyamaina Magesa.

Mashindano ya SHIMIWI mwaka huu yanachezwa kwa mara ya 34 tangu kuasisiwa kwake na mkoa wa Morogoro umeepewa heshima ya kuandaa mashindano hayo kwa mara nyingine ambapo iliwahi kuandaa mashindano hayo mwaka 2009, 2012 na 2014.

No comments:

Post a Comment