Wednesday, October 13, 2010

Mapacha watatu kuzindua album yao ya kwanza Ijumaa hii

Habari za kazi wadau,

Natumaini mtakuwa mnawajua vijana wa Mapacha Wa3 ambao ni Khalid Chuma a.k.a Chokoraa, Kalala Hamza a.k.a Kalala Junior wote kutoka bendi ya Twanga Pepeta na mimi mwenyewe Joseph Mponezya a.k.a Jose Mara wa FM Academia Tunatarajia kuzindua album yetu ya kwanza iitwayo "Jasho la Mtu" Album itazinduliwa tarehe 15 Octoba 2010 katika ukumbi wa Travertine - Magomeni kuanzia saa 3 usiku kwa kiingilio cha Tshs. 10,000/- tu.

 pia tutasindikizwa na The African Stars (Twanga Pepeta) Full squad na Mfalme wa Taarab nchini Mzee Yusuf.

Naombeni msaada wenu wa kunitangazia kwenye blog zenu.

Shukrani.

Jose Mara

No comments:

Post a Comment