Saturday, September 7, 2013

TAMASHA LA 'MTAKUJA' SEPT 14


Usikose tamasha la “Mtakuja” kwa Wanafunzi Jumamosi, Septemba 14

 Picture
Baada ya muda mrefu kupita bila kuwa na tamasha lolote la wanafunzi hasa wa shule za Sekondari, uongozi wa Mtakuja Secondary School ya Kunduchi kwa kushirikiana na mtangazaji maarufu Allan Lucky 'Rais wa Wanafunzi' wa kipindi maarufu cha Skonga ambacho hurushwa kupitia televisheni ya vijana ya EATV umeandaa tamasha la wanafunzi linalotarajiwa kuhudhuriwa na wanafunzi zaidi ya 3,000 kutoka katika shule zaidi ya 20 za jijini Dar-es-Salaam.

Tamasha hilo lenye lengo la kuwakutanisha wanafunzi wa shule mbali mbali za Dar-es-Salaam kwa pamoja na kupata changamoto kimawazo na kiburudani, pia kuwakutanisha wadau mbalimbali wa elimu katika
kufanikisha uboreshwaji wa elimu na kusaidia katika kutekeleza mpango wa 'Matokeo Makubwa Sasa', linatarajiwa kufanyika Jumamosi ijayo tarehe 14/09/2013 katika viwanja vya shule hiyo.

Miongoni mwa shule ambazo zitashiriki ni: Mtakuja, Kondo, Jordan, St. Gasper, Mbezi Beach, Boko, Goba, Twiga, Maendeleo, Mwambao, Kisauke, Kinzudi, londa, Makongo, Kawe Ukwamani, Tegeta, Mbweni, Teta, Hananasif na Mtongani, zote ni za sekondari.

Tamasha hilo linatarajiwa kuhusisha wadau mbali mbali wa elimu watakaokutana katika kubadilishana mawazo na kupata burudani kwa kushuhudia vipaji lukuki walivyo navyo wanafunzi kutoka shule mbali mbali.

Miongoni mwa shughuli zitakazoendeshwa ni pamoja na maswali na majibu, fashion show, uimbaji, ufokaji, na wanafunzi wenye vipaji mbali mbali maalum watapewa nafasi.

Msemaji wa tamasha hilo ambaye pia ni mwalimu wa michezo wa Mtakuja Beach Sekondari Bw Misonji Charles amewataka wadau mbali mbali wa elimu kuhudhuria na kushuhudia vipaji vya wanafunzi mbali mbali na pia amewataka waandishi wa habari kujitokeza kwa wingi katika kuchukua habari na matukio mbali mbali yatakayojitokeza. Pia amewaomba wadau mbali mbali wenye uwezo wa kuchangia katika kufanikisha tamasha hili wajitokeze, kwa kuwa linaandaliwa kwa nguvu za shule na kamati maalum ya maandalizi pekee.

Kwa maelezo na kama unataka kushiriki, tafadhali wasiliana na Msemaji wa Tamsha Bw Misonji Charles kupitia 0714642442

No comments:

Post a Comment