Tuesday, July 29, 2014

TIMU Y ATAIFA YA MCHEZO WA CHESS YAKABIDHIWA BENDERA YA TAIFA KWA AJILI YA KUSHIRIKI MASHINDANO YA KIMATAIFA NCHINI NORWAY

       

Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (kulia), akimakabidhi Bendera ya Taifa, mmoja wa wachezaji wa timu ya Taifa wa mchezo wa Chess, Hemed Mlawa (wa pili kushoto), Dar es Salaam leo asubuhi kwa ajili ya kuondoka kesho kwenda kushiriki mashindano ya kimataifa nchini Norway. Wa pili kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini, kushoto ni mchezaji Emmanuel Mwaisumbe. Safari hiyo imedhaminiwa na Tanzania Chess Foundation na Kasparov Foundation.
Hapa ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (katikati), Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini (kulia), mchezaji Hemed Mlawa (kushoto) na Emmanuel Mwaisumbe (wa pili kushoto), wakifurahi baada ya kucheza mchezo huo wakati wakiwaonesha waandishi wa habari.
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (katikati), akizungumza na wanahabri kabla ya kukabidhi bendera. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini na kulia mchezaji Hemed Mlawa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini, akizungumza na wanahabari. Kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini, akizungumza na wanahabari.
Wachezaji wa mchezo huo, Hemed Mlawa (kulia) na Emmanuel Mwaisumbe wakiwa kwenye hafla hiyo ya kukabidhiwa bendera ya Taifa. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania, Henry Lihaya.
Kulia ni Mratibu wa Chess Tanzania, Johnson Mshana akifuatilia kwa karibu tukio hilo. Kushoto ni Mwanahabari
Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi (katikati), akizungumza na wanahabri kabla ya kukabidhi bendera. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini na kulia mchezaji Hemed Mlawa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet, Vinay Choundry ambaye ni muasisi wa mchezo huo hapa nchini na mchezaji wa mchezo huo, Hemed Mlawa wakionesha umahiri wa kucheza mchezo huo mbele ya wanahabari.Katikati ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT), Dioniz Malinzi na mchezaji Emmanuel Mwaisumbe. (Imeandaliwa na www.habari za jamii.com- simu namba 0712-727062, 0786-858550)
…………………………………………………………………………………………..
Dotto Mwaibale
 
TIMU ya Taifa ya Chess imeagwa Dar es Salaam leo asubuhi kwajili ya kwenda kushiriki mashindano ya chess 41 ya kimataifa Olympiads yatakayofanyika nchini Norway.
 
Jumla ya wachezaji watano wataondoka nchini leo usiku kwenda kushiriki mashindano hayo.
 
Wachezaji hao ni Geofrey Mwanyika, Hemed Mlawa, Emmanuel Mwaisumbe, Nurdin Hassuji na Yusuph Mdoe.
 
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi timu hiyo bendera ya taifa, Mwenyekiti wa Baraza la Michezo Tanzania, Dioniz Malinzi alisema kuwa kuwakabidhi bendera hiyo ni ishara ya kuwatakia safari njema na ushindi katika mashindano hayo.
 
Malinzi alisema anashukuru wale wote ambao wamekuwa katika mstari wa mbele kusimamia mchezo huo nchini hadi kufikia kushiriki mashindano ya kimataifa.
 
”Namshukuru sana Mr Vinay kwa msaada wake anaoutoa kusapoti mchezo huu Tanzania na kwa moyo wake wa kutoa, maana waswahili husema kutoa ni moyo na sio utajiri maana kuna matajiri wegi lakini sio watoaji” alisema
 
Aliongeza kuwa anamatumaini kuwa wachezaji hao watakwenda kufanya vizuri katika mashindano hayo na kuitangza Tanzania.
 
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Spicenet na Mwanzilishi wa Mchezo wa Chess Tanzania, Vinay Choudary alisema kwa yeyote atakayeweza kuibuka na ubingwa shilingi milioni mia moja zitatolewa kwa ajili yake.
 
Choudary alisema hadi sasa walipofikia ni pazuri kwa Tanzania kushiriki mashindano ya kimataifa hivyo anawatakia safari njema na ushindi katika mchezo huo.
 
Mchezaji Hemed Mlawa alisema wataiwakilisha vema Tanzania na watahakikisha wanafanya vizuri.
 
”Hii ni mara ya kwanza sisi kushiriki hivyo hatuwezi kusema kuwa tutarudi na ushindi moja kwa moja bali tutafanya vizuri na tunaamini tunaweza kuzishinda baadhi ya nchi”alisema
 
Mashindano hayo ni ya wiki mbili na yameratibiwa na Shirikisho la Chess Duniani(FIDE)
na kudhaminiwa na Tanzania Chess Association na Kasparov Association.

No comments:

Post a Comment