Monday, March 12, 2012

Lema na Zitto kivutio kampeni za Chadema Arumeru


Godbless Lema amekuwa kivutio kikubwa alipowasili jana hapa Usa river majira ya saa saba na nusu mchana kutokea Arusha. Alikuwa na maandamano makubwa ya magari,pikipiki,na waenda kwa miguu. Alipokaribia tu kufika vijana wa hapa walimbeba juu wakati wote na kufunga barabara kwa muda mpaka walipompeleka sehemu ambako wageni wanafikia. Baadaye  maandamano makubwa ya kupokea viongozi watakaozindua kampeni yakafuata
  
Mh Zitto Kabwe akiwasili eneo la tukio.
Umati wa watu ukiwa unaelekea eneo la mkutano katika viwanja vya shule ya Msingi Leganza.
Waendesha pikipiki hawako nyuma kama wanavyoonekana katika picha hii.
Barabara za kutokea Moshi na Arusha zimefurika watu wakija kwenye uzinduzi wa CHADEMA.
Picha na Habari na Mdau Maalum Wa Maggid Mjengwa-Arumeru

No comments:

Post a Comment