Tuesday, March 20, 2012

Basi la Prince Muro lapata ajali Usiku wa kuamkia Leo Tunduma

Basi la Kampuni ya Prince Muro lenye namba za usajili T 485 BQV lililokuwa likifanya safari yake ya kutoka Dar es Salaam kuelekea Tunduma mkoani Mbeya limepoata ajali na kupinduka usiku wa kuamkia leo.

Ajali hiyo iliyotokea wakati dereva wa basi hilo akijaribu kulipita Lori katika maeneo ya Senjele wakati likielekea Tunduma na kusababisha kifo cha mtu mmoja na kujeruhi wengine 14.

Hivi ndivyo zinavyo onekana Damu na viti kuharibika vibaya baada ya ajali hiyo iliyo tokea jana usiku

Baadhi ya mabaki ya vitu baada ya ajali hiyo jana usiku

Hili Ndilo Gari la mizigo ambalo basi la Price muro lilitaka kulipita, na  baadae kushindwa na kupinduka baada ya kukutana na Gari lengine mbele yake


Shimo hili limechimbika wakati wa ajali hiyo ilipo tokea jana usiku.
Picha zaidi  MBEYA YETU BLOG

No comments:

Post a Comment