Friday, March 16, 2012

Mazishi ya Mwakilishi jimbo la Bububu Zanzibar yafanyika leo



Mamia ya wananchi wa Zanzibar kesho asubuhi wanatarajiwa kushiriki katika mazishi ya aliekuwa Mwakilishi wa Jimbo la BUBUBU Marehemu Salum Amour Mtondoo aliefariki Dunia leo katika Hospitali mkuu ya Mnazi Mmoja Mjini Zanzibar baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kichwa. 
 
 Kwa mujibu ya ratiba ya shughuli za Mazishi iliotolewa na Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Zanzibar imeeleza kuwa mnamo sasa tatu za asubuhi maiti ya Marehemu itaondoka Mijini kuelekea Bumbwini Kijijuini kwao kwa kusaliwa na baadae kuzikwa. 
 
 Katika Mazishi hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohamed Aboud atasoma risala na baadae Baraza la Wawakilishi Zanzibar itatoa risala yake itakayosomwa na Spika wa Baraza hilo Pandu Ameir Kificho na baadae Familia ya Marehemu Salum Amour Mtondoo itatowa tamko la shukrani. 
 
 Tangu Uchaguzi Mkuu Kumalizika wa Mwaka 2010 huyu atakuwa Mwakilisdhi wa pili kufariki Dunia ambapo Mwakilishi wa kwanza kufariki ni Mwakilishi wa Jimbo la Uzini ambae pia alikuwa Mbunge aliechaguliwa na Baraza la Wawakilishi Marehemu Mussa Khamis Silima wote hao wawaili ni kutoka chama cha Mapinduzi.

No comments:

Post a Comment