Friday, February 10, 2012

BEACH BORA RESORT “a new era of leisure & entertainment”KUZINDULIWA LEO



Kiwanja cha maraha cha Beach bora resort kinatarajiwa kuzinduliwa jioni ya leo tarehe 10.02.2012 baada ya kubinafsishwa na kupata uongozi mpya.Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mjini Bagamoyo asubuhi ya leo kutoka kwa mkurugenzi  wa Beach bora resort bw. Mussa Maganga uzinduzi huo utatawaliwa na burudani kutoka kwa madj wa maarufu wa mjini Bagamoyo.

“Tunatarajia shughuli yetu kuanza saa 12:00 jioni na ninawahakikishia wageni waalikwa wote huduma ya hali ya juu na usalama wa kutosha” alisema Maganga.

Beach bora resort yenye mandhari nzuri ipo kwenye ufukwe wa bahari ya Hindi mjini  Bagamoyo na inapakana kwa karibu kabisa na Taasisi ya sanaa na utamaduni Bagamoyo(Tasuba).

No comments:

Post a Comment