Thursday, January 5, 2012

HAMAD RASHID ATIMULIWA CUF

 
Mbunge wa Wawi kwa tikeri ya CUF, Hamad Rashid Mohammed (pichani) amefukuzwa katika chama hicho.          

Taarifa zilizopatikana jana, zimesema Hamadi ambaye pia ni Mjumbe wa Baraza Kuu CUF, amefukuzwa pamoja na viongozi wengine kadhaa akiwemo Mjumbe wa Baraza Kuu mkoa wa Tanga, Doyo Hassani.

      Wengine waliokumbwa na fagio hilo la kutimuliwa ni Hamis Shoka (Mjumbe wa Baraza Kuu, Pemba), Juma Sanaani (Mjumbe wa Baraza Kuu la Chama hicho, wakati Mjumbe wa Baraza Kuu Mbeya Yassin Mrotwa amepigwa bonge la karipio au karipio kali.

      Katika makali yake ya kujivua gamba, taarifa zimesema wanachama wengine ambao si wajumbe wa Baraza kuu, walitarajiwa kuhojiwa ili kuchukukiwa hatua.

        Kwa mujibu wa Katiba ya CUF, Hamadi na wengine waliofukuzwa wanayo fursa ya kukata rufani  kwenye mkutano mkuu wa Taifa wa chama hicho.

No comments:

Post a Comment