Monday, January 30, 2012

TWIGA STARS YAICHAPA NAMIBIA MAGOLI 5-2 UWANJA WA TAIFA

Mchezaji Mwanahamisi Omari a.k.a Gaucho akihojiwa na mwandishi wa habari wa BBC Eric David Nampesya baada ya kumalizika kwa mpira kati ya Twiga Stars na Namibia , Mwanahamis Omari 'Gaucho' ni mfungaji pekee wa mabao 2 kati ya 5 ya Twiga, katika mchezo wa kutafuta kufuzu kwa fainali za Afrika kwa Wanawake, zinazotarajia kufanyika mwezi Juni mwaka huu.
Mchezo huo umemalizika muda mchache katika uwanja wa Taifa.
Mabao ya Twiga yalifungwa na Mwnahamisi Omar katika dakika 21, Asha Rashid 'Mwalala', bao la pili dakika 46, bao la tatu Etoe Mlenzi, dakika ya 84, Asha Rashid,bao la nne dakika ya 88, na bao la tano, likifungwa tena na Mwanahamis, dakika ya 90. Mabao ya Namibia mawili ya yamefungwa na Beki wa Twiga, Etoe, aliyejifunga dakika ya 29 na bao la pili likifungwa na Juliana Skrywer, dakika 73.
Kwa matokeo hayo sasa Twiga Stars inatarajia kukutana na mshindi kati ya Misri au Ethiopia ambapo Misri ilikuwa inaongoza kwa mabao 4-2 dhidi ya Ethiopia.
Mchezaji wa timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania Twiga Stars Asha Rashid akimtoka beki wa timu ya taifa ya Namibia ya wanawakeLovisa Mulunga, katika mchezo wa kuwania fainali za kombe la dunia kwa wanawake unaochezwa kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam jioni hii,
Wachezaji wa Twiga Stars wakishagilia mara baada ya mchezaji wa timu hiyo Asha Rashid kufunga goli la pili katika kipindi cha pili.
Mashabiki wakiimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa mpambano huo kwenye uwanja wa Taifa.

No comments:

Post a Comment