Thursday, January 5, 2012

Kundi la Boko Haram lashambulia mji wa Maiduguri


Mashambulio mawili ya mabomu yametokea katika mji wa Maiduguri kaskazini mwa Nigeria yakiwa ndio machafuko ya kwanza kutokea tangu kutangazwa kwa hali ya hatari mjini humo.
Hakuna majeruhi yaliyoripotiwa katika ghasia hizi zinazodhaniwa kutekelezwa na wapiganaji wa kundi la kiislam lilopigwa marufuku la Boko Haram.
Kundi hilo linawataka waumini wa dini ya kikristo kutoka kusini mwa nchi hiyo waishio kaskazini mwa nchi kuondoka mara moja.

Msichana auawa

Awali, msichana mmoja aliuawa wakati wa ufyatulianaji wa risasi katika ya wapiganaji wanaoaminika kuwa wa kundi hilo la Boko Haram na maafisa wa polisi katika jimbo la Jigawa.
Jumapili iliyopita kundi hilo la Boko Haram lilitoa makataa kwa watu kutoka jamii ya wakristo kusini mwa Nigeria, waondoke maeneo ya Kaskazini mwa nchi.
Rais Goodluck Jonathan ametangaza hali ya hatari katika majimbo manne nchini humo.

Mgomo juu ya ruzuku ya mafuta

Mashambulio hayo yanatokea huku maandamano kupinga kuondolewa kwa ruzuka ya mafuta ya petroli yakiendelea.
Katika eneo la Liberation Square mjini Kano , maafisa wa polisi nchini humu wametumia gesi ya kutoa machozi na virungu kuwatawanya wanafunzi waliokuwa wakiandamana katika eneo lilowazi kupinga kuondolewa kwa ruzuku ya mafuta.
Makundi ya kutetea haki za binadamu yameshutumu kitendo hicho cha polisi.
Aidha, Raia nchini humo wamechukizwa na tangazo la serikali hapo Jumapili kwamba itaondolewa ruzuku hiyo ambayo inaigharimu serikali mamilioni ya dola katika mapato.

No comments:

Post a Comment