Thursday, December 29, 2011

BENDI TANO ZILIZONIKUNA MWAKA 2011


African Stars Twanga pepeta bado wako kileleni kwa kushika namba moja kutokana na nyimbo zao walizoziipua hivi karibuni za "Dunia daraja" utunzi wa Charles baba na"Penzi la shemeji" ya kwake Muumini Mwinjuma
Extra Bongo wazee wa kizigo wameshika namba mbili kutokana na Umahiri wao wawapo stejini lakini pia kwa nyimbo zao za "Mtenda akitendewa" na "Fisadi wa mapenzi"

Bendi changa kabisa hapa Bongo ya Mapacha watatu nayo imeshika namba tatu kutokana na Wimbo wao Shika ushikacho na Gari bovu utunzi wa mpiga kinanda wao Erasto Mashine
Salute kwao Akudo Impact kwa nuimbo zao "Umefulia" na "Umejificha wapi" ambazo zimewapa nafasi ya tatu katika chati hii
Fm Academia "wazee wa Ngwasuma" wameshika nafasi ya tano kwa nyimbo zao Heshima kwa mwanamke na Usiku wa giza

Jamani huu ni mtazamo wangu tuu inawezekana na wewe una Bendi zako ambazo unaona zimekukuna zaidi...kwa hiyo masela msijenge chukiiii!! hahahaha
 
Chanzo Afrokija 

No comments:

Post a Comment