Friday, December 23, 2011

TBL YATOA MSAADA WA SARUJI SHULE ZA MBEYA


Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) Mkoa wa Mbeya Calvin Martin (kulia) akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro sehemu ya mifuko ya saruji kati ya 200 yenye thamani ya sh.milioni 3,iliyotolewa na kiwanda hicho juzi kwa ajili ya ujenzi wa madarasa ya shule mbalimbali mkoani humo.Wa pili kutoka kushoto ni Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa TBL Edith Mushi na Meneja Mauzo na Usambazi wa TBL Kanda ya Kusini, James Kavuma.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro akisalimiana na Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa TBL Edith Mushi mara baada ya kuwasili kukabidhiwa saruji hiyo.


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (kushoto) akitoa shukurani kwa uongozi wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) baada ya kupokea msaada huo.Kulia ni Meneja UHusiano na Mawasiliano wa TBL Edith Mushi na Meneja Mauzo na Usambaji wa TBL Kanda ya Kusini James Mavuna na Meneja wa Kiwanda cha Bia Mkoa wa Mbeya Calvin Martin.

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Abbas Kandoro (kushoto),akisalimiana na Meneja wa Kiwanda cha Bia Tanzania (TBL) Mkoa wa Mbeya Calvin Martin mara baada ya kuwasili juzi viwanja vya Uwanja Mpya wa Ndege Songwe kwa ajili ya kukabidhiwa saruji na upandaji miti kazi iliyoratibiwa na TBL. TBL ilitoa mifuko 200 ya saruji kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa madarasa katika mkoa huo.
Baadhi ya wananchi wa mkoa wa Mbeya na wale wanaozunguka uwanja mpya wa ndege wa Songwe na wafanyakazi wa TBL walioshuhudia tukio hilo.

No comments:

Post a Comment