Thursday, December 29, 2011

HALIMA MCHUKA HATUNAE TENA DUNIANI



Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji Tanzania, TBC – HALIMA MCHUKA amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI Jijini DSM alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa kiharusi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa TBC CLEMENT MSHANA, HALIMA MCHUKA alikimbizwa katika hospitali ya DAR GROUP na baadae katika hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI hapo jana baada ya kuanguka ghafla akiwa katika kituo chake cha kazi eneo la PUGU ROAD Jijini DSM.

MCHUKA alikuwa mtangazajii wa kwanza wa kike wa mpira AFRIKA MASHARIKI.

BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.
 AMINA

chanzo Jane john 

No comments:

Post a Comment