Monday, April 2, 2012

AIRTEL YAANZA SHAMRA SHAMRA ZA SIKUKUU KWA KUSHEREKEA NA WATOTO


 Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania wakijumuika kwa pamoja na  watoto  wa wafanyakazi wa Airtel katika shamra shamra tamasha maalum la watoto kuelekea kusheherekea sikukuu ya pasaka kwa michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini Dar-es-salaam kwa hisani ya Airtel.
 Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania wakijumuika kwa pamoja na  watoto  wa wafanyakazi wa Airtel kukakata keki iliyoandaliwa na kampuni ya Airtel Tanzania katika shamra shamra za tamasha maalum kuelekea sikukuu ya pasaka ambapo watoto hao walipata nafasi ya kucheza  michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini Dar-es-salaam.
 Meneja mauzo wa kampuni ya Airtel Tanzania Bi.Hilda Nakajumo akikata keki kwa  pamoja na Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania na watoto  wa wafanyakazi wa Airtel katika shamra shamra za  kuelekea sikukuu ya pasaka ambapo watoto hao walipata nafasi ya  kucheza michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini Dar-es-salaam.
 Mkurugenzi wa Biashara  wa kampuni ya Airtel Tanzania Bw.Irene  Madeje akizungumza na waandishi wa habari katika sherehe ya michezo kwa Watoto wa wateja wa kampuni ya Airtel Tanzania na  watoto wa wafanyakazi wa kampuni hiyo katika shamra shamra za  kusheherekea sikukuu ya pasaka na kuendeleza uhusiano mzuri uliopo kati ya wateja wa Airtel na wafanyakazi wa Airtel ambapo watoto hao walipata nafasi ya  kucheza  michezo mbali mbali kwa pamoja  ambayo imefanyika katika kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini Dar-es-salaam.
Watoto wakicheza mchezo wa kuendesha magari wakati wa tamasha maalum la michezo kwa watoto lilioandaliwa na Airtel ili  kutoa nafasi kwa watoto  wafanyakazi wa Airtel pamoja na watoto wa wateja wa Airtel jijini Dar esa salaam kukutana na kucheza  michezo mbali mbali kwa pamoja, tamasha hilo  lililofanyika katika kituo cha michezo ya watoto kiitwacho Fun Sport  ndani ya jengo la Qualty center Jijini Dar-es-salaam kwa udhamini wa  Airtel .
---
Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel yaanza shamrashamra za sikukuu kwa kujumuika na watoto wa wateja wao jijini Dar es saalam ambapo watoto zaidi ya 150 walipata nafasi ya kukutana pamoja jumamosi mwishoni mwa wiki hii  katika ukumbi wa Quality Center - Fun sports na kufurahi kwa pamoja.
.
Huu ni mkakati ambao Airtel imejiwekea  kusherehekea pamoja na watoto wa wateja wao wa makapuni ( corporate customer)  wiki moja kabla ya sikukuu za pasaka huku lengo likiwa ni kuwa karibu na wateja wao na kusambaza upendo wa kampuni hiyo kwa wateja wake na familia zao.

Akiongea kwa niaba ya Airtel Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Bi Irene Madege alisema" leo tunajisikia furaha kuwa na watoto wa wateja wetu na kujumuika nao pamoja, Tumekuwa tukifanya shughuli mbalimbali ikiwa ni katika kuwazawadia wateja wetu, lakini leo tunatumia muda huu kuwapa burudani watoto ambao ndio wateja wetu wa kesho".

Kwa muda wa takribani masaa 4 watoto zaidi ya 150 walipata burudani mbalimbali ikiwa pamoja na michezo mbalimbali ya watoto kama face painting, mashindano ya kucheza music, na pia kupata nafasi ya kukutana na wafanyakazi wa Airtel,  kumzungumza pamoja na kuwasisitiza watoto kuwa wasikivu shuleni ili  kufanya vizuri kwenye masomo yao, tunaamini watoto hawa wamekuwa na wakati mzuri pamoja nasi. Aliongeza Bi Irene.

No comments:

Post a Comment