Wednesday, April 18, 2012

RAIS KIKWETE MKUTANONI BRASILIA, BRAZIL

 Ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Open Government Partnership ukibadilishana mawazo kabla ya ufunguzi wa mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil, April 17, 2012. kutoka kushoto ni  Waziri katika  ofisi ya Rais (Utawala Bora) Mh  Mathias Chikawe,  Waziri wa kazi na Uwezeshaji Wanachi Kiuchumi na Ushirika wa Zanzibar Mh Haroun Ali Suleiman, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh Mahadhi J. Maalim na Msahuri wa Rais (Masuala ya Siasa) Dkt Laurian Ndumbaro
   Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akiwa meza kuu na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff  na wajumbe wengine katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil, April 17, 2012 wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership. Kulia ni Waziri wa mambo ya Nje wa Marekani Bi Hilary Clinton
 Wajumbe wa Tanzania kutoka taasisi mbalimbali za kiraia na serikali wakiwa katika  ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil, April 17, 2012 wakati wa ufunguzi wa mkutano wa Open Government Partnership
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akihutubia katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil, April 17, 2012 katika mkutano wa Open Government Partnership 
 Rais Dkt Jakaya Mrisho Kikwete akilakiwa na mwenyeji wake Rais wa Brazil Mama Dilma Rousseff alipowasili katika ukumbi wa mikutano wa Brasilia Convention Centre jijini Brasilia, Brazil, April 17, 2012 kuhudhuria mkutano wa Open Government Partnership 

Picha na ikulu

No comments:

Post a Comment