Wednesday, April 4, 2012

SIMBA YAWASILI SALAMA NCHINI ALGERIA.

Wekundu wa Msimbazi Simba sports club wamewasili mjini Algiers hivi leo wakitokea jijini Cairo walikokuwa wameweka kituo chao cha siku moja wakiwa njiani, kuelekea kwenye mchezo wa marejeano wa michuano ya kombe la shirikisho barani Afrika.
Simba, itashuka Stade 8 May 1945 mjini Setif kuwakabili wenyeji Entente Sportive Setifienne ya Algeria, kwenye mchezo wa marejeano wa michuano hiyo, ikiwa na akiba ya ushindi wa mabao mawili kwa sifuri uliopatikana kwenye uwanja wa nyumbani jijini Dar es salaam, siku nane zilizopita.
Taarifa toka mjini humo zinasema kwamba, wawakilishi hao pekee wa Tanzania katika michuano ya kimataifa, wamefika salama na kukaa uwanja wa ndege kwa masaa mawili kabla ya kupokelewa na watanzania wachache waishio mjini Algiers. 

Nae mwenyekiti wa klabu ya Simba Muheshimiwa Ismail Aden Rage ambae ameongozana na timu hiyo pia akiwa mkuu wa msafara anasema kwamba wanasikitika sana kutokana na kuwekwa uwanja wa ndege kwa muda wa masaa mawili.
Aden anasema kwamba, pia wamekuwa na malumbano na wenyeji wao juu ya usafiri wa kutoka mjini Algiers hadi mji utakaochezwa mchezo huo, kwani kutokana na umbali walilazimika wapannde ndege lakini haikuwa hivyo.
Hata hivyo, pamoja na matatizo ya hapa na pale hasa tukio la kuzuiliwa kwa kamera ya mwandishi wa Clouds FM Sports Xtra Geofrey Leah, Aden anasema kwamba jambo hilo amelisimamia kidete ili kuliweka sawa, lakini pia anashukuru kwa mapokezi ya Watanzania wachache waliopo mjini Algiers.

No comments:

Post a Comment