Tuesday, April 24, 2012

MAFUGULI ASHIRIKI KUUAGA MWILI WA MUASISI WA CHAMA CHA MAPINDIZI WA WILAYA YA CHATO

                                   Waziri Magufuli akitoa salamu za mwisho

 
Waziri wa Ujenzi Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Chato leo ameshiriki kuuaga mwili wa Marehemu Constantine Jaha Misungwi ambaye ni muasisi wa Chama cha Mapinduzi wilayani Chato.
 
Marehemu Misungwi alizaliwa tarehe 01 Julai mwaka 1925 ambapo katika muda mwingi wa uhai wake alikuwa akijihusisha sana na shughuli za kisiasa. Marehemu Misungwi ndiye mwanzilishi wa mji wa Chato na katika nyakati tofauti aliwahi kushika nafasi mbali mbali ikiwamo ya Uenyekiti wa Chama cha Mapinduzi katika mji wa Chato, Udiwani na pia Uenyekiti wa Chamba Cha Mapinduzi katika Jimbo la Biharamulo Mashariki.
Marehemu mzee Misungwu ndiye aliyemshawishi Mheshimiwa Magufuli kujiunga na siasa mnamo mwaka 1990 na baadaye kumchukulia tena fomu za kugombea Ubunge wa Jimbo la Biharamulo Mashariki mwaka 1995 na kushinda kwa mara ya kwanza.
Mmoja ya watoto wa marehemu, Bwana Kaloli ameelezea kuwa baba yake alilazimika kuletwa Dar es Salaam kutokea Chato kwa ajili ya matibabu ya kansa na alilazwa kwa wiki mbili katika Hospitali ya Tumaini kabla ya kuruhusiwa kutoka mnamo tarehe 20 Aprili 2012 lakini hata hivyo mauti yakamfika siku mbili baadaye akiwa nyumbani kwa mwanaye huyo.Mwili wa Marehemu Mzee Misungwi umesafirishwa leo kuelekea Chato kwa mazishi

No comments:

Post a Comment