Tuesday, April 10, 2012

Wabunge Nassari na Cecilia wa CHADEMA 'wasepa' kuapishwa hii leo

Wabunge wawili wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, wote kutoka Mkoani Arusha waliokuwa waapishwe hii leo mjini Dodoma wajaripoti Bungeni hapo.

Taarifa iliyosomwa na Spika wa Bunge, Anna Makinda asubuhi hii baada ya kufungua Mkutano wa Bunge ulioanza leo mjini Dodoma inasema kuwa Wabunge hao Joshua Nasari wa Arumeru Mashariki na Mwingine wa Viti Maalum ambaye amemrithi Marehemu Regia Mtema Cecilia Daniel Pareso, hawajatokea Bungeni mjini Dodoma hii leo.


Cecilia kabla ya uteuzi huo wa Chadema alikuwa ni Diwani wa Kata ya Qurus, iliyoko katika Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, mkoani Arusha.


Kwa Mujibu wa Spika Wabunge hao watapaswa kukutana na Kamati ya Bunge ya Uongozi na watapangiwa tarehe nyingine ya kuapishwa.

Wabunge hao walipaswa kuapishwa hii leo kabla ya kuanza kwa shughuli za Bunge.
FK Blog itaendelea kufuatilia habarii hii ili kujua sababu za kuto kufikaa kwao Bungeni hii leo.

No comments:

Post a Comment