Wednesday, April 4, 2012

SAMATTA KUKAA ZAIDI NJE KWA MAUMIVU YA BEGA


MSHAMBULIAJI chipukizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Ally Samatta anaweza kuwa nje ya Uwanja kwa muda zaidi kutokana na maumivu yake ya bega aliyoyapata wiki iliyopita mjini Kitwe Zambia, akiichezea klabu yake Tout Puissant Mazembe dhidi ya Power Dynamos ya huko katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Taarifa kwenye tovuti ya TPM imesema leo kwamba, Samatta akiwa Kenya alilazimika kusimama kwa muda kutokana na kuzidiwa kwa maumivu na hiyo inamaanisha hataweza kucheza mechi ya Jumapili dhidi ya Dynamos.
Samatta aliyefunga bao la Mazembe katika sare ya 1-1 ugenini kwenye mechi hiyo ya kwanza, Raundi ya Pili Ligi ya Mabingwa Afrika, sasa hataweza kucheza mechi ya marudiano Jumapili.
TP Mazemebe imepata pigo linguine, mchezaji wake kufuatia kifo cha baba wa mchezaji wao, Francis Kalala ‘Postolo’, Kasongo Ngongo aliyezaliwa mwaka 1946.

No comments:

Post a Comment