Monday, April 2, 2012

Anguko La CCM Arumeru : Tafsiri Yangu


Ndugu zangu,
Unaweza kuwatawanya watu kwa mabomu , lakini kamwe, mabomu hayawezi kuitawanya mioyo ya watu yenye kutaka mabadiliko.

Habari kubwa usiku wa kuamkia leo ni anguko la CCM kuleArumeru Mashariki kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha Ubunge.

Tafsiri yangu;

Kuna wakati Rais Mstaafu Benjamin Mkapa alipata kutamka; " CCM haina hati miliki ya kutawala". Mkapa aliusema ukweli wake ambao kwa bahati mbaya hupata tabu kuusimamia. Na hakika, idadi ya Watanzania wenye kutaka mabadiliko inazidikuongezeka.  Na katika siasa za nchi hiiukiona wanawake watu wazima wanashiriki mikutano ya kampeni ya wapinzani, basi,ujue ni ishara ya mabadiliko yanayokuja.

Na ukweli mwingine ni huu; vijana wengi zaidi wamekuwa mstari wa mbele katika kutakamabadiliko hayo.  Kimsingi ArumeruMashariki wamechagua mabadiliko. Na si kwamba Chadema ni chama bora na makinisana, la hasha, Watanzania wengi zaidi  vijana wanaonyesha kuichukia CCM. Miongonimwao ni Wana-CCM.  Kiukweli, mvuto wa ChamaCha Mapinduzi kwa Watanzania na hususan vijana unazidi kupungua.

Na ajabu ya matokeo ya Arumeru?

Katika hali isiyo ya kawaida, kuna Wana- CCM waliyoyapokeakwa furaha matokeo ya chama chao kushindwa Arumeru. Tafsiri yake?  Ni kushamiri, si tu kwa makundi ndani ya chamahicho, bali, hofu ya kutokea kwa mpasuko ndani ya chama hicho katika mbio zakuusaka Urais ifikapo mwaka 2015.

Kitakachotokea sasa ndani ya chama hicho ni ‘ Witch hunting’-kutafutana uchawi. Bila shaka, kuna maswali yatakayoulizwa. Moja kubwa ni hili;kimeshindwa chama  au mgombea? Na msukumowa swali hilo ni katika kumtafuta mchawi na kukitenganisha chama na mgombeakatika ‘Anguko la Arumeru’.  Huo utakuwani mwendelezo wa ‘ Vita vya Panzi’ ndani ya CCM. Lakini, katika siasa, kunawanaoamini pia, kuwa wakati mwingine kuna lazima ya kuwepo kwa ‘ Vita vya Panzi’ili kujitenganisha na kumbikumbi.

CCM ifanye nini?

Jibu; ifuate njia ya Dr Harrison Mwakyembe

Akizungumza na mamia ya wananchi wa Kata ya Ipinda  hivi majuzi Dr Mwakyembe alitoa kwa watu wake kauli ya ‘ Kichifu’ na iliyojaa hekimana busara. Alisema; “ Mimi sikubaliani na mtu yeyote anayesema kitu cha kwanzani chama  chako…. Hapana, mimi kitu chakwanza  kwangu siyo CCM , cha kwanza mimini Mtanzania, cha pili ndio tunaingia kwenye vyama. Mtu anayekimbilia chamakuwa cha kwanza hivi hicho chama kingetokea wapi kama siyo taifa?”. ( Dr HarrisonMwakyembe, Nipashe, Machi 31, 2012)

Na nilimwona na kumsikia Dr. Mwakyembe akiyasema hayo kwenyeruninga.  Umati ule uliomshangilia DrMwakyembe ulikuwa wa wananchi bila kujali itikadi zao. Kulikuwa na Wana -Chademapia, na kiongozi wa Chadema alipewa kipaza sauti kuongea kumkaribisha ‘ ChifuMwakyembe’ aliyerudi nyumbani na mtazamo mpya wa kizalendo.

Kuifuata njia ya Mwakyembe itawasaidia CCM kurudishaumaarufu wao. Maana,  moja ya sababu za wananchiwalio wengi kuichukia CCM ni hulka yake ya kuwabagua wapinzani na kuwaona niwatu wasiofaa kushiriki uongozi wa nchi.

WaTanzania wengi sasa wanatambua, kuwasi kweli wapinzani ni watu wabaya. Ni maadui. Kwamba watasababisha vita navurugu. Wananchi wameona pia kazi njema inayofanywa na upinzani. Ghiliba hii yaCCM kuwachonganisha wapinzani kwa wananchi imepitwa na wakati. Badala yake,inachangia kupunguza kura za CCM.

Na CCM isipobadilika sasa, na Chadema ikabaki kama ilivyosasa bila kusambaratika, basi, CCM  itakuwa na wakati mgumu sana ifikapo 2015,maana, kuna ‘Jeshi kubwa’ la vijana linalojiandaa na kushiriki uchaguzi wa2015.  Jeshi hili linaundwa na vijanawengi wasio na ajira wala hakika ya maisha yao ya kesho. Wanaiona CCM kamasehemu ya matatizo yao. Wana kiu ya kumpata mkombozi.



Na wanafunzi hawa wa Shule za Kata wamegeuka kuwa ‘agitators’ wazuri wa mabadiliko. Ikumbukwe, shule za kata ziko vijijini. Sikuhizi hata  waliokuwa wakiitwa ‘ wajinga’wa vijijini wamepata walimu wa kuwafungua macho. Watoto wao wenyewe wanaosomaau waliomaliza shule za kata na kubaki vijijini kwa vile hata uwezo wakujisomesha elimu ya juu hawana. Hawa hawana mapenzi na CCM.

Na katika vijana mia moja hii leo, utapata kazi kubwakuwapata 20 wanaoipenda CCM. Huundio ukweli wa hali halisi. CCM ibadilike na kuwa chama cha kisasa kilichotayari hata kuongoza nchi pamoja na wenzao wa upinzani. Yumkini jitihada za CCMkuangamiza upinzani zaweza kuwa na madhara makubwa endapo CCM itapata bahatimbaya ya kuondolewa madarakani 2015. Maana, anguko hilo laweza pia kumaanisha kifo cha chama hicho.
 
CCM haipaswi sasakufikiria mikakati ya kuangamiza upinzani ili watawale daima. Dhana ya ’ CCMDaima’ ni ndoto iliyopitwa na wakati. Katika Tanzania ya sasa kuna wengi wenyekuombea  kubaki hai na kushiriki kuzifutandoto kama hizo.

CCM ya sasa inapaswa kupanga mikakati yakuendelea kuongoza dola huku ikishirikiana hata na wapinzani. Ingawa hata huoni mtihani mgumu wenye kukihitaji chama hicho kuwa na watu makini zaidi badalaya waendekeza fitina na majungu.

Na hii ni tafsiriyangu.

Maggid Mjengwa,
Iringa
0788 111 765
http://mjengwablog.com

No comments:

Post a Comment