Sunday, August 14, 2011

KAMANDA MAYUNGA AZIKWA


Maafisa wa Jeshi la Wananchi wakibeba jeneza lenye mwili wa marehemu Luteni Jenerali Silas Mayunga kuelekea kaburini tayari kwa mazishi yaliyofanyika Agosti 12, 2011 Nyumbani kwake Maswa Mkoani Shinyanga na kuhudhuriwa na Viongozi mbalimbali akiwepo Rais Jakaya Kikwete.
Maafisa kutoka Jeshi la Wananchi wakishusha jeneza lililohifadhi mwili wa Marehemu Luteni Jenerali Silas Mayunga kaburini.
Rais Jakaya Kikwete akiongoza mamia ya waombolezaji waliohudhuria mazishi ya marehemu Luteni Jenerali Silas Mayunga nyumbani kwake huko Maswa mkoani Shinyanga.
Rais Jakaya Kikwete na mkewe Salama Kikwete wakiweka shada la maua katika kaburi la Luteni Jenerali Silas Mayunga

No comments:

Post a Comment