Saturday, August 13, 2011

KCB YAAGWA VIONGOZI WAKE


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya KCB Tanzania Edmund Mndolwa (kushoto) akimkabidhi zawadi ya ngao Mkurugezi wa Benki hiyo anayemaliza muda wake, Joram Kiarie baada ya kuitumikia wa kipindi cha miaka 6 katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa KCB  Kenya, Peter Muthoka (kulia)  Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa KCB Tanzania, Edmund Mndolwa na Mkurugenzi wa Benki ya KCB Tanzania Joram Kiarie wakibadilishana mawazo wakati wa hafla ya kuwaaga  baadhi ya Wakurugenzi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya KCB Tanzania Edmund Mndolwa akizungumza.
Mwenyekiti wa Bodi  ya Wakurugenzi wa Benki ya KCB na Baadhi ya Wakurugenzi wa benki hiyo wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa hafla ya kuwaaga baadhi ya wakurugenzi wa benki hiyo jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Masoko na Mahusiano wa KCB Tanzania Christine Manyenye  akiwa na moja ya zawadi ambayo alikabidhiwa mmoja ya Wakurugenzi  wa benki hiyo  wakati wa hafla ya kuwaaga baadhi ya wakurugenzi wa benki  jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment