Friday, August 19, 2011

MUSTAFA HASSANALI ASHIRIKI MAONESHO BOTSWANA

Mbunifu wa Kiafrika, Mustafa Hassanali nchini Botswana,Gaborone

Mbunifu Mustafa Hassanali,ndio alikua mtanzania pekee aliealikwa kuwakilisha nchi yake katika wiki ya kwanza ya Fashion Botswana, iliyofahamika kama Color in the desert fashion week.

Hafla hii,iliudhuliwa na wabunifu mbalimbali wa kimataifa na wenyeji.Baadhi ya wabunifu wa kiafrika walioudhulia walikua , Taibo Bacar (Mozambique), David Tlale,na Thula Sindi kutoka Afrika kusini, Moo Cow (Kenya), Joyse Nyasha Chimanye( Zimbabwe). Kauli mbiu ya Fashion week mwaka huu,ilikua "Kuongeza tija na maendeleo ya fani ya ubunifu wa mavazi na viwanda vya nguo Botswana"

Mustafa Hassanali alisema "Kutokana na uzoefu wangu,Botswana ni nchi yangu ya kumi na moja kiafrika na ya kumi na tatu kidunia kufanya maonesho ya ubunifu,Na nnajisikia faraja na kujivunia kuwa mmoja wa walioudhulia week ya kwanza ya fashion Botswana,na pia kuwa mmoja wa kuendeleza uhusiano mzuri kati ya Tanzania na Botswana kupitia Fashion "

No comments:

Post a Comment