Tuesday, August 9, 2011

VIMWANA WA MISS TANZANIA 2011 WAPIGWA MSASA

 Warembo wanao wania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakifuatilia mafunzo katika semina maalum ya warembo hao inayoendelea katika Hotel ya Giraffe Ocean View iliyopo Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Warembo hawa baada ya kumalizika semina hii watahamia katika Jumba la Vodacom House.

Mkurugenzi wa Lino International Agency, Waandaaji wa Miss Tanzania, Hasim Lundenga (katikati) akifafanua jambo wakati wa semina maalum kwa washiriki wa Vodacom Miss Tanzania 2011. Kulia ni Mkurugenzi wa Ukuzaji Sanaa kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Nsao Shalua na kushoto ni Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania Prashant Patel.

Warembo wakiunga mkono hoja kwa kuipigia makofi. Warembo 30 wapo kambini kwaajili ya kujifua na mchuano huo utakao fanyika mwezi Septemba jijini Dar es Salaam.

Wanyange hawa leo watapandaa jukwaani katika shindano dogo la kumsaka Miss Top Model. Mrembo ambaye moja kwa moja atapata tiketi ya kuingia nusu fainali za Miss Tanzania.

No comments:

Post a Comment