Monday, October 31, 2011

KATIBU MKUU WA WIZARA YA AFYA, BLANDINA NYONI AFUNGA KONGAMANO LA WANAHABARI LA UTAFITI WA HUDUMA ZA AFYA ZA NHIF


Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni (kushoto) akizungumza na wanahabari baada ya kufunga kongamano la wahariri na waandishi wa habari waandamizi kuhusu taarifa za tafiti za upatikanaji wa huduma za afya zilitolewazo na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) nchini. Kongamano hilo la siku mbili lilifanyika mjini Morogoro.
Blandina Nyoni akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Clement Mshana.
Mkurugenzi Mkuu wa NHIF, Emmanuel Humba akitoa majumuisho ya mapendekezo yaliyotolewa na wadau kwenye kongamano hilo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Blandina Nyoni (kushoto), akipongezwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), Dk. Emmanuel Humba baada ya kufunga kongamano la wahariri na waandishi wa waandamizi wa habari la kujadili taarifa za tafiti za upatikanaji wa huduma za afya zinazotolewa na mfuko huo nchini.Kongamano hilo la siku mbili lilifanyika, mjini Morogoro. Katikati ni Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Deo Mtasiwa. (PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA)
Mwenyekiti wa Kongamano hilo, Lauden Mwambona akiongoza mijadala ya tafiti hizo. Kutoka kushoto ni Benny Mwaipaja wa TBC Manyara na Saiboko wa Daily News.
Mhariri Mtendaji wa New Habari, Deodatus Balile akichangia hoja wakati wa kongamano hilo. kushoto ni Mussa Juma wa Mwananchi Arusha.
Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Clement Mshana akichangia hoja wakati wa kongamano hilo
Joyce Mwakalinga wa Stars Tv na Margareth Tengule wa Star TV wakishiriki kongamano hilo
Cosmas Nadimi wa MSD, akijibu maswali mbalimbali ya wanahabari kuhusu usambazaji wa dawa nchini
Abdul Saiboko wa Daily News, akitoa taarifa ya utafiti wa bima ya afya Mkoa wa Kilimanjaro. Kushoto ni Mtafiti mwenzie, Masanja wa Star Tv, Kilimanjaro
Mwandishi wa habari wa gazeti la Mtanzania, Cloudia Karedia akiwa kazini
Mtangazaji wa TBC Tabora Nico Mwaibale akitoa taarifa ya utafi huo kwa Mkoa wa Tabora. Kulia ni mtafiti mwenzie, Vedasto Msungu wa ITV.
George Marato wa ITV, Mara, akifafanua jambo wakati wa kongamano hilo
Baadhi ya washiriki wakiwa katika kongamano hilo mjini Moro.

No comments:

Post a Comment