Monday, October 31, 2011

USIKU WA BAGAMOYO INTERCOLLEGES NIGHT 2011 WAIBAMBA BAGAMOYO

Mwakikishi kutoka taasisi ya sanaa na utamaduni Tasuba bibie Fatma Kihemba akitoa salam za chuo chake kwenye usiku wa Bagamoyo Intercolleges Night 2011 uliyofanyika kwenye ukumbi wa Tasuba mjini Bagamoyo siku ya Ijumaa tarehe 28.10.2001.
Mdau Rabia kulia akifuatilia matukio ya Bagamoyo Intercolleges Night 2011.

Bw.Kim Kimenya mkurugenzi wa kampuni ya Kimkev Entertainment akitoa neno la makaribisho.

Rais wa wanachuo wa Tasuba bw.Gasper Tesha akiwasilisha mada juu ya umuhimu wa kozi ya sanaa na utamaduni kwa jamii.
Mdau akiuliza swali kwa mtoa mada wa Tasuba.
Mtoa mada kutoka SLADS bw. Godfrey Assenga akiwasilisha mada juu ya umuhimu wa kozi ya ukutubi na utunzaji wa nyaraka.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya KG Son kutoka TMK wanaume halisi akishambulia jukwaa.
Shabiki wa burudani na taaluma akijaribu kujibu swali la usiku wa Bagamoyo Intercolleges Night 2011.
Mkurugenzi Kim Kimenya akimkabidhi fedha taslimu bibie Manka mshindi wa swali la usiku wa Bagamoyo Intercolleges Night 2011.
Haji Adam (Baba Haji) akihost shughuli nzima ya Bagamoyo Intercolleges Night 2011.

Mkurugenzi wa kampuni ya Mrimi Classic wear bw Gesase Mrimi akitanganza zawadi kwa "lady of the night" bibie Aisha Kiputula (kushoto) na Francis Kamuli "man of the night"(katikati) wote kutoka SLADS(walichaguliwa kwa kigezo cha kupendeza kwa nguo za rangi nyeupe).

Bw.Martin Mhando kutoka taasisi ya utafiti ya Ifakara mara baada ya kumtangaza Aisha Kiputula kuwa ndiye Lady of the night.

Picha ya pamoja ya washindi na waandaaji.Washindi walipata zawadi za fedha taslimu na kulala usiku mmoja katika hoteli ya Green pack village ya Bagamoyo.
Huu ulikuwa wakati wa wote yaani kwanja time.

No comments:

Post a Comment