Monday, November 28, 2011

WAREMBO WAWILI MISS UTALII TANZANIA 2010/2011 KWENDA UTURUKI DISEMBA 19 2011








Mshindi wa tano wa fainali za taifa za Miss Utalii Tanzania2010/2011 Sophia Dio na mshindi wa taji la vipaji la Miss Utalii Tanzania 2010/2011 Dessy Mushumbuzi,wanatarajia kuondoka nchini 19-12-2011 ,kwenda kuwakilisha Tanzania katika mashindano ya Dunia ya Miss Globe International 2011.

Jumla ya nchi 120 Duniani zinashiriki katika shindano hilo,litakalofanyika 30-12-2011 katika jiji la Istanbul na kuonyeshwa Live kupitia TV mbalimbali Duniani. Shindano hilo kama lilivyo shindano la Miss Utalii Tanzania,linalenga kutangaza na Utalii,Utamaduni wa mataifa mabalimbali Duniani,pia kuunganisha na kubadilishana tamaduni miongoni mwa mataifa na washiriki.


Hii itakuwa ni fulsa nyingine kwa Tanzania kuweza kutangaza utalii na utamaduni wetu kimataifa, na hata mianya ya uwekezaji iliyopo Tanzania kupitia warembo hawa wa Miss Utalii Tanzania, ambao historia inaonyesha kuwa mara zote wanaposhiriki mashindano ya Dunia na kimataifa hutwaa mataji mbalimbali. hadi sasa Miss Utalii Tanzania tunashikilia zaidi ya mataji 5 ya Dunia,yakiwemo Miss Tourism World 2005- Africa, Miss Tourism World 2006 -SADC, Miss Tourism World 2007 - Africa, Model Of The World 2008 - Personality , Miss Africa 2006 - !ST Runner Up n.k


Tunaendelea na maandalizi kuhakikisha tunadumisha na hata kuvuka rekodi ya kwa kuahalilisha kuwa warembo hao wanarudi na mataji na sio wasindikizaji kama walivyo wengine. Tunaomba makampuni na watu mabalimbali wajitokeze kudhamini na kuchangia safari na ushiriki wa warembo hao katika mashindano hayo ya Dunia

No comments:

Post a Comment