Saturday, August 2, 2014

AFCON 2015: MALAWI NA RWANDA ZAFUZU HATUA YA MAKUNDI KWA PENATI

other
 
MALAWI wamefuzu hatua ya makundi ya kuwania tiketi ya kucheza fainali za mataifa ya Afrika, AFCON 2015 nchini Morocco baada ya kuifunga Benin kwa mikwaju 4-3 ya penalti.
Mechi iliyopita mjini Cotonou, Malawi walifungwa bao 1-0 na leo wakiwa nyumbani wamepata ushindi wa aina hiyo, hivyo sheria ya mikwaju ya penalti kutumika kuamua mshindi.
Bao pekee la ushindi kwa Malawi liligungwa na John Banda katika dakika ya 13.
 Malawi ambao wapo nafasi ya 16 kwa nchi za Afrika katika viwango vya FIFA walitawala mchezo kwa muda mrefu, lakini walishindwa kupata mabao mpaka penalti zikaamua.
Benin ndio walikuwa wa kwanza kulishambulia lango la Malawi, lakini nyota wake Stephane Sessegnon alikosa nafasi kadhaa na kuipa Malawi kupata faida ya ushindi kwa penalti.
Baada ya ushindi huo, Malawi watakabiliana na nchi za Mali, Ethiopia na Algeria kwenye kundi B.
Wakati huo huo, Rwanda nao wamefuzu hatua ya makundi kwa mikwaju ya penalti baada ya kufuta kipigo cha mabao 2-0 walichopata ugenini dhidi ya Congo-Brazzavile.
Mabao mawili ya Rwanda yalifungwa kipindi cha pili kupitia kwa Ndahinduka Michel katika dakika 55 na Meddy Kagere katika dakika ya 60 na kuipa nchi hiyo ushindi.

Rwanda walishinda penati 4-3 na Patrick Sibomana alifunga penati ya ushindi na sasa wanaungana na mabingwa watetezi Nigeria, Afrika kusini na Sudan katika kundi A.

No comments:

Post a Comment