Friday, August 1, 2014

SIMBA SC YAMTAMBULISHA RASMI ELIAS MAGURI NA SHABAN KISIGA ‘MALONE’

                    

NYANGE
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
SIMBA SC imewatambulisha wachezaji wawili iliyowasijili majira haya ya kiangazi kwa mujibu wa mahitaji ya kocha mkuu, Mcroatia Zdravko Logarusic.
Makamu wa Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema zoezi la usajili linakwenda vizuri na amewatambulisha Shaaban Kisiga `Malone` aliyesajiliwa kutoka Mtibwa Sugar na Elias Maguri kutoka Ruvu Shooting.
“Zoezi la usajili bado linaendelea kwa kuwa muda unaruhusu. Zoezi hili linaendelea kwa taratibu na kwa umakini, wengine wanaweza kusema kuna ucheleweshaji au ugoigoi, usajili ni jambo makini linalohitaji kufanywa kwa umakini mkubwa,” alisema Kaburu.
“Zoezi hili linakwenda vizuri na kamati ya usajili inafanya kazi kwa ukaribu sana na benchi la ufundi kupitia mwalimu wetu mku,”
“Na leo hii tumekuja kuwatambulisha rasmi wachezaji wawili ambao simba imewasajili,”
“Mchezaji wa kwanza ni Shaban Kisiga, uwezo wake mnaufahamu, ni mchezaji wa kimataifa, alishachezeaSimba huko nyuma, akaenda kimataifa na akarudi Mtibwa na kusaini miaka miwili na sasa anarudi nyumbani. Mchezaji wa pili ni Elias Maguri kutoka Ruvu Shooting”.
Baada ya kutambulishwa, Shaaban Kisiga kwa apande wake alisema:
“Nashukuru kwa kurudi klabu yangu ya Simba, nawashukuru viongozi na kocha. Nina imani nitafanya vizuri na kuisaidia timu.”
Kwa upande wake Maguri alisema: “Ninashukuru kujiunga na Simba, najua ni timu kubwa yenye changamoto nyingi, kazi yangu sio kuongea bali ni vitendo uwanjani.”
Elias Maguri amesaini mkataba wa miaka miwili kuitumikia klabu ya Simba.

No comments:

Post a Comment