Saturday, September 6, 2014

NEYMAR AITENDEA HAKI BEJI YA UNAHODHA, ATANDIKA KIDUDE BRAZIL IKISHINDA 1-0 DHIDI YA COLOMBIA



Goalscorer: Neymar (right) celebrates after scoring Brazil's winning goal against Colombia in Friday's 1-0 win

Mfungaji: Neymar (kulia) akishangilia baada ya kuifungia  Brazil goli la ushindi dhidi ya Colombia jana usiku.

NEYMAR akiwa nahodha wa Brazil kwa mara ya kwanza amefanikiwa kufunga bao pekee katika ushindi wa 1-0 dhidi ya Colombia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliopigwa mjini Miami.
Hii ilikuwa mechi ya kwanza tangu Brazil wafanyiwe kitu mbaya na Ujerumani kwa kufungwa mabao 7-1 katika mchezo wa nusu fainali wa kombe la dunia na 3-0 katika mchezo wa mshindi wa tatu dhidi ya Uholanzi.
Ushindi wa jana ni faraja kubwa kwa kocha Dunga aliyerithi mikoba ya Luiz Felipe Scolari aliyefungashiwa virago baada ya kuvurunda  katika fainali za kombe la dunia zilizomalizika mwezi julai mwaka huu nchini Brazil.
Katika mchezo wa jana nyota wa Manchester United , Radamel Falcao alitokea benchi, lakini ni habari njema kwa Lousi van Gaal kwasababu nyota huyo alikaa nje ya uwanja kwa muda mrefu kutokana na majeruhi.
Captain fantastic: Neymar, pictured with Juan Zuniga, skippered Brazil against Colombia in Miami

Nahodha mkali: Neymar, alipigwa picha akimuonesha ufundi mbaya wake Juan Zuniga.


Karudi: Radamel Falcao alicheza dakika 15 tu  dhidi ya  Brazil
Making a point: Manchester United's new striker Radamel Falcao gestures to the fans ahead of kick-off

Kikosi cha Brazil: Jefferson, Maicon, Miranda, Luiz (Marquinhos, 80), Luis, Gustavo (Fernandinho, 46), Ramires (Elias, 46), Oscar (Everton Ribeiro), Willian (Coutinho, 72), Diego Tardelli (Robinho, 77), Neymar. 
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Rafael Cabral, Danilo, Gil, Marcelo, Goulart.
Mfungaji wa goli: Neymar, 82.
Kadi ya njano: Ramires, Luiz GustavoBooked:

Kikosi cha Colombia: Ospina, Zuniga (Mejia, 73), Zapata, Valdes Parra, Armero, Cuadrado, Ramirez (Arias, 46), Sanchez (Ramos, 85), Rodriguez (Falcao, 77), Martinez (Guarin, 65), Gutierrez (Bacca, 64)
Wachezaji wa akiba ambao hawakucheza: Vargas, Valencia, Aguilar, Ibarbo, Balanta, Ramos, Quintero, Carbonero, Muriel.
Kadi ya njano: Cudrado, Sanchez, Zuniga, Valdes, Gutierrez.
Kadi nyekundu: Cuadrado. 
Watazamaji: 73,429 
Mwamuzi: Dave Gantar 

No comments:

Post a Comment