Tuesday, September 13, 2011

16 waenda Afrika Kusini katika Mashindano ya Guinness Footabal Challenge

WAKONGWE WA SOKA OKOCHA, DESAILLY, SONG NA BWALYA KUWANAO PAMOJA KATIKA GUINNESS FOOTBALL CHALLENGE

Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Epraim Mafuru akizungumza katika mkutani na waandishi wa Habari Dar es Salaam juzi juu ya timu nane ambazo zina mashabiki 16 wa mpira wa miguu wanaokwenda nchini Afrika Kusini katika mashindano ya Guinness Football Challenge. Timu hizo zinaondoka Septemba 13, 2011 leo. Pamoja nae anaeonekana Kulia ni Meneja wa Chapa ya Guinness, Maurice Njowoka.
Meneja wa Chapa ya Guinness, Maurice Njowoka (kulia) akifafanua jambo kuhusiano na mashindano hayo. Pamojanae ni Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Epraim Mafuru.Vijana hao walipatikana katika mchujo maalum wiki iliyopita katika viwanja vya Leaders Club na vijana hao wanatarajia kurejea nchini September 26,2011 na wakiwa huko mbali na kufundishwa soka la kimataifa pia watashiriki katika kuandaa matangazo mbalimbali ya GFC.
Mkurugenzi wa Masoko wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Epraim Mafuru (katikati) akizungumza katika mkutani na waandishi wa Habari Dar es Salaam na kuwataja wachezaji wakongwe wa Afrika watakao kuwa na vijana hao kwa nyakati tofauti Afrika Kusini kuwa ni Jay Jay Okocha, Kalusha Bwalya, Marcel Desailly na Rigobert Song.  Pamoja nae Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa SBL, Teddy Mapunda na meneja wa chapa ya Guiness,Maurice Njowoka

No comments:

Post a Comment