Friday, September 30, 2011

Nyarandu na Mrema wawapongeza Polisi na TRA Moshi kukamata Sukari.


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu( Kulia),Mbunge wa Vunjo Mh Augustine Mrema ( Katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Moshi Mussa Samisi wakizungumza na vyombo vya Habari mara baada ya kutazama sukari iliyokamatwa katika maeneo ya mipakani Mkoani Kilimanjaro.
Baadhi ya mifuko ya sukari iliyokamatwa ikiwa imehifadhiwa katika ghala la Polisi kituo cha Polisi Himo Mkoani Kilimanjaro.
Mkuu wa Kituo cha poliosi Himo Afande Majura( Kushoto) akimuonyesha Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalanmdu na Mbunge wa Vunjo Mh Mrema baadhi ya magari yaliyokamatwa yakiwa na bidhaa mbali mbali za magendo ikiwemo sukari.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu( Kushoto), akijibu hoja mbali mbali za Mbunge wa Vunjo Mh Augustino Mrema (Kulia) alipokuwa katika ziara yake ya kutembelea Masoko na vituo vya biashara mipakani kastika Mkoa wa Kilimanjaro. Wanaoshuhudia ni viongozi na watendaji wa Mamlaka mbali mbali katika Mji Mdogo wa Himo.
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Mh Lazaro Nyalandu akitoa maagizo kwa watendaji wa mamlaka mbali za serikali katika Mji mdogo wa Himo mara baada ya kukamilisha ziara yake ya kutembelea na kukagua masoko na vituo vya Biashara mipakani katika Mkoa wa Kilimanjaro

No comments:

Post a Comment