Wednesday, September 21, 2011

TANZANIA YAPATA TUZO YA DUNIA YA AFYA,TEKNOLOJIA NA MAENDELEO

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa Grameen Bank Bhaban ya nchini Bangladesh Professor Muhammad Yunus mara baada ya kikao cha majadiliano kuhusu wanawake na maendeleo ya kilimo yaliyofanyika huko Nwe York wakati wa kikao cha 66 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa tarehe 19.9.2011.
Rais Jakaya Kikwete akifurahia tuzo ya Global Health,Technology and Development mara baada ya kukabidhiwa na Mwenyekiti wa South-South Awards 2011 Mheshimiwa Winston Baldwin Spencer, Waziri Mkuu wa Antigua and Barbuda (kulia) katika sherehe iliyofanyika katika hoteli ya Waldorf Astoria jijini New York tarehe 19.9.2011
Rais Jakaya Kikwete akishiriki katika majadiliano na baadhi ya viongozi mashuhuri duniani kuhusu wanawake na maendeleo ya kilimo duniani (Women and Agriculture. A conversation on improving Global food security.) Mkutano ulioandaliwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Hillary Clinton katika hoteli ya Intercontinental Barclay jijini New York katika siku ya kwanza ya kikao cha 66 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (United Nations General Assembly) tarehe 19.9.2011.
Rais Jakaya Kikwete akiwahutubia marais na Wakuu wa nchi mbalimbali duniani walioshiriki katika sherehe ya utoaji tuzo hizo wakati wa kikao cha 66 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York nchini Marekani tarehe 19.9.2011.

No comments:

Post a Comment