Friday, September 16, 2011

MKENYA AINGIA UWANJANI AKIWA UCHI WA MNYAMA




Jamaa mmoja mwenye asili ya kenya aliingia uwanjani akiwa uchi wa mnyama kwenye mechi kati ya England na Argentina kwenye michuano ya Rugby World Cup - 2011 inayofanyika nchini New Zealand .

Inasemekana jamaa ni mzaliwa wa Kenya ana miaka 23 na alikua hajavaa kitu zaidi ya kuchora uso wake,na alikatiza kwenye uwanja wa Otago na kuonekana na mamilioni ya watazamaji wa television duniani,baadaye alikamatwa na wana usalama na huenda akakabiliwa na kifungo che miezi 3 jela au faini ya dola 5,000.
Wachambuzi wa mambo wanadai kuwa jamaa huyo aliamua kufanya hivyo ili kujizolea umaarufu duniani.

No comments:

Post a Comment