Friday, September 23, 2011

MAANDALIZI YA SENSA YA MAJARIBIO YAANZA


Mkufunzi kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu Bi. Neema Ngure akitoa ufafanuzi  wa fomu za dodoso zitakazotumika kwenye sensa ya majaribio ya watu na makazi 2011 kwa wafanyakazi watakaosimamia zoezi hilo litakalofanyika mwezi ujao katika maeneo mbalimbali nchini wakati wa semina ya mafunzo leo mjini Morogoro.
Wafanyakazi watakaosimamia zoezi la sensa ya majaribio ya watu na makazi 2011 kutoka  maeneo mbalimbali nchini wakifanya mtihani wa kupima uelewa leo mjini Morogoro wakati wa semina ya mafunzo ya usimamizi wa zoezi la sensa litakalohusisha maeneo ya mikoa ya Dar es salaam, Kanda ya ziwa, Kanda ya kati, mikoa ya kusini na nyanda za juu kusini pamoja na Zanzibar.

No comments:

Post a Comment