Sunday, September 11, 2011

SALHA ISRAEL NDIYE MISS VODACOM TANZANIA 2011


Hatimaye kitendawili cha "Nani Vodacom Miss Tanzania 2011" kilichokuwa kikigonga vichwa vya wadau wengi wa urembo sasa kimetenguliwa baada ya Miss Ilala 2011, Salha Izrael kunyakua taji la Vodacom Miss Tanzania 2011.

Salha ambaye nyota yake ilianza kungaa tangu kuingia katika kambi hiyo na kuanza minong'ono ya hapa na pale kuwa ndiye anaestahili kuvaa taji hilo alitawazwa kuwa malkia mpya waTanzania baada ya kuwabwaga warembo wengine 29 katika shindano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

Salha mrembo aliyeanza harakati zake za Vodacom Miss Tanzania katika kitongoji cha Dar City Centre na kubahatika kunyakua nafasi ya pili kitongojini hapo na baadae kunyakua taji la Ilala. 

Pia mrembo huyu naweza kumuita Miss Chalinze 2011 baada ya vijana wengi wafanyao biashara katika njia panda ya Segera na Morogo pale Chalinze kumtabiria kuwa mshindi baada ya kumuona wakati wa safari ya kutembelea mbuga za wanyama Kanda ya Kaskazini. 

Kwa Ushindi huo wa kuamkia leo Salha amefanikiwa kuvaa taji Miss Tanzania 2011 alilokuanalo Genevieve Mpangala na kujipatia zawadi ya gari aina ya Jeep lenye thamani ya Tsh 72milioni pamoja na kitita cha Sh Milioni 8.

Nafasi ya pili ilikwenda kwa Trace Mabula ambaye pia anashikilia taji la Miss Photogenic na nafasi ya tatu ikienda kwa Miss Pesonality 2011, Alexia Willium.
Warembo waliofanikiwa kuingia hatua ya 5 bora ya Vodacom Miss Tanzania 2011 wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka kushoto ni Miss Sports Woman, Loveness Flavian, Miss Photogenic Tracy Mabula, Jenifa Kakolaki, Miss Personality, Alexia Willium na Salha Izrael

No comments:

Post a Comment