Friday, September 23, 2011

Watanzania wafanya vyema GFC Afika Kusini


Na Mwandishi Wetu TIMU ya Tanzania inayoshiriki kwa mara ya kwanza kwenye mashindano ya kujibu maswali na kupiga mipira yanayojulikana kama Guinness Mpira Chanagmoto yanayoendelea huko Johannesburg Afrika Kusini, wamefanya kufuru isiyotegemewa baada kuongoza mapaka hatua ya tano hapo juzi. 
Kinyang’anyiro hicho kinachoshirikisha jumla ya washiriki 50, 16 wakiwa ni Watanzania na waliobaki ni washiriki wa Kenya na Uganda, kinaendelea hadi hapo kesho kitakapofikia mwisho wa hatua la nane. 
Mpaka jana kabla ya hatua ya sita timu ya George Lukuba na Freddy Jordan ndio waliokuwa vinara kwa kujinyakulia kiasi kizuri cha pesa. Vijana hao walishinda katika hatua za tatu na nne za kinyang’anyiro hicho wakati Sultan Mohamed na Mansoor Seif walikuwa wapili baada ya kina Lukuba. 
Vijana hao wa Kitanzania ambao walionekana kuyumba katika hatua ya mazoezi yaliyofanyika kwa siku mbili katika studio za kisasa za Q ( Q-Studios) zilizopo huko Kew, mpakani na kitongoji cha Alexandra ambacho ni cha pili kwa kukaliwa na Wazalendo wengi wa asili ya Kiafrika baada ya Soweto kwa jiji la Johannesburg, wamewashangaza waandaazi wa changamoto hiyo ya mpira wa miguu. 
Watanzania hao wamekuwa wepesi kujibu maswali na kupiga mipira na kuwabwaga Waganda ambao walianza kwa mbwembwe nyingi wakati wa mazoezi.
Lukuba amesema wao nia yao ni lushinda kuvuta fuba (pesa) hayo yanayotolewa na watengenezaji wa kinywaji cha Guinness ambacho kinasambazwa na Kampuni ya bia ya Serengeti hapa nchini. 
Vijana hao walifanyiwa usaili wiki mbili zilizopita katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam, walipanda ndege kuelekea Johannesburg siku ya Jumanne wiki liyopita. Jumla ya hatua nane zinashindaniwa katika kinyang’anyiro hicho ambacho kina toa dola elfu hamsini kila hatua. 
Lukuba ambaye tuliwasiliana naye moja kwa moja jana alisema ndoto ya washiriki wa Kitanzania ni kuendela kuvuta pesa ili kuubwaga umasikini na kuwatoa nishai wenzao wa Kenya na Uganda ambao wamekuwa wakiwabeza kabla ya mashindano kuanza. 
Changamoto hiyo ya Guinness itaoneshwa na televisheni inayopendwa na watazamaji wengi nchini, ITV kwa wiki nane mfululizo. Washindi wa hatua zote nane watajiunga na wanasoka wannne waliostafu soka katika onyesho ambalo pia litashirikisha watazamaji ambao watatuma ujumbe mfupi wa maandishi kupitia simu zao za mkononi kujaribu bahati yao ya kuvuta pesa hapo baadaye. 
Wachezaji hao ni Jay Jay Okocha wa Nigeria, Rigobert Song wa Cameroon, Kalusha Bwalya wa Zambia na Mfaransa Marcel Desaily aliyekuwa beki mahiri wa timu ya Chelsea na Ufaransa iliyoshinda kombe la Dubnia mwaka 1998. Desaily kwa sass anaishi Accra, Ghana. Hii imekuwa fursa pekee kwa Watanzania kujiongezea kipato kupitia onyesho hilo. 
Labda habari za kusikitisha ni kuhusu mshiriki mmoja wa Kitanzania Juma Nassoro ambaye anaumwa jipu juu ya paja lake la kushoto ambalo limepasuka na anaendelea vizuri. 
Mshiriki mwingine wa Uganda Daniel Elagon amebanwa na malaria tokea siku ya Jumamosi wakati wa hatua ya mwanzo ambapo kulikuwa na baridi kali jijini Johannesburg. Shindano hili la Guinness limekuwa likifanyika katika nchi za Ghana na Cameroon pia Kenya na Uganda walikuwa washiriki kwa mara ya kwanza mwaka jana na hii ni mara yao ya pili. 
Washiriki hao wanatarajiwa kurejea Dar es Salaam siku ya Jumapili kwa ndege ya shirika la ndege la Afrika Kusini saa moja jioni.

No comments:

Post a Comment