Friday, September 23, 2011

WAHARIRI WAPIGWA MSASA KUHUSU HAKI ZA BINADAMU


Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Masaju akifungua semina ya Wahariri wa Vyombo vya habari nchini iliyolenga kuwafahamisha kuhusu kusaidia kuandika habari juu ya haki za binadamu. Semina hiyo imeandaliwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa kushirikiana na Umoja wa Mataifa nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Masuala ya mahusiano ya Katiba na Haki za Binadamu kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. Mathew Mwamu.
Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alberic Kacou hotuba ya Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw. George Masaju wakati wa Ufunguzi wa Semina ya siku moja ya wahariri wakuu wa vyombo vya habari (TANZANIA EDITORS' FORUM) iliyofanyika katika hoteli ya Double Tree by Hilton jijini Dar es Salaam.
Wahariri Wakuu wa Vyombo mbalimbali vya habari nchini wakifuatilia mada zilizokuwa zikitolewa na watoa mada katika Hoteli ya Double Tree By Hilton jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Bw. Alberic Kacou akibadilishana mawazo na Mhariri wa Makala wa Gazeti la Serikali la kila siku (Daily News) Deogratius Mushi.

No comments:

Post a Comment