Tuesday, September 13, 2011

300 WAFA KATIKA MILIPUKO YA MAFUTA KENYA NA CONGO DRC

ZAIDI ya watu 330 wamefariki dunia  katika matukio mawili ya kulipuka kwa mafuta ambapo tukio la kwanza liliua watu100 nchini Kenya.Habari kutoka Jijini Nairobi zilisema watu hao walifariki baada ya bomba la mafuta kulipuka na kusababisha moto uliosambaa na kuwaunguza watu wengi.

Wakati hali ikiwa ya majonzi nchini Kenya, nayo Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo(DRC), ilipata pigo baada ya watu 230 kuteketea kwa moto kufuatia tukio la lori lililobeba mafuta kulipuka nchini humo.Moto huo uliua watu hao na wengine wengi kujeruhiwa  na kwamba vyombo vya usalama vya nchi hiyo vilikuwa kikiendelea kuokoa watu wengine.
Habari zaidi kutoka Kenya zilisema mlipuko wa bomba la mafuta ulisababisha moto mkubwa  katika eneo la viwanda mjini hapo, na kuwaunguza watu wengi ambao miili yao hadi sasa haijatambuliwa.  Hata hivyo, Jeshi la Polisi nchini humo lilisema idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka na kuwa zaidi ya 100.  Waandishi wa Gazeti  Mama la Mwananchi, Daily Nation, waliokuwapo eneo la tukio, waliwahesabu watu 73 ambao walikuwa wamefariki dunia.

 Mashuhuda walisema, bomba hilo la mafuta  ya petroli linatumiwa kusafirisha mafuta katika nchi za jirani na Kenya.   Habari zinasema, licha ya vikosi vya zimamoto kuendelea kuuzima moto huo kwa kasi, miili ya watu wengi iliharibika vibaya.  Idadi kubwa ya majeruhi walipelekwa hospitalini na magari ya dharura ambayo yalikuja kwa wingi baada ya tukio hilo.  Habari zaidi za matukio hayo soma ukurasa wa 14.

Chanzo: Gazeti la Mwananchi

No comments:

Post a Comment