Friday, September 23, 2011

Malinzi Mwenyekiti Mpya BMT


Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Mheshimiwa Dkt. Emmanuel John Nchimbi (Mb) amemteua Bw. Dionis Malinzi kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT).
Aidha pia amewateua wafuatao kuwa Wajumbe wa Baraza la Michezo la Taifa.
    1. Mhe. Jenister Mhagama (Mb)
    2. Mhe. Mkiwa A. Kimwanga (Mb)
    3. Bw. Jamal Rwambow
    4. Bw. Venance Mwamoto
    5. Bw. Juma Pinto
    6. Dkt. Cyprian Maro
    7. Bw. Kanali Eliot Makafu
    8. Bibi Jeniffer Mmasi
    9. Bw. Ramadhani Dau
    10. Bw. Alex Mgongolwa
    11. Bw. Maulid Kitenge
Wengine ni Wajumbe wa kuteuliwa kutokana na nafasi zao:
Mkurugenzi Mkuu - Bodi ya Michezo ya Kubahatisha
Kamishna wa Elimu - Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Mwakilishi - TAMISEMI
Mkurugenzi wa Michezo – Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo.
Mwakilishi - Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali.
Wajumbe kutoka Wawakilishi wa Vyama vya Michezo (Makatibu) ni:
CHANETA - Chama cha Netiboli Tanzania
TPC - Tanzania Paralympic Committee
AAT - Automobile Association of Tanzania
TSA - Tanzania Swimming Association
BFT - Boxing Federation of Tanzania
RT - Riadha Tanzania
TFF - Tanzania Football Federation
TBF - Tanzania Basketball Federation
TOC - Tanzania Olympic Committee
TTTA - Tanzania Table Tennis Association
 
Uteuzi huu umefanywa kwa kuzingatia Mamlaka ya Waziri chini ya kifungu cha 3(2) cha nyongeza ya Katiba ya Sheria ya BMT Na. 12 ya mwaka 1967 na marekebisho yake katika Sheria Na. 6 ya mwaka 1971.
Wajumbe hao watalitumikia Baraza kwa kipindi cha miaka mitatu.
Imetolewa na Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo
22.09.2011

No comments:

Post a Comment