Tuesday, September 20, 2011

TBL yachangia waathirika wa ajali ya Meli Zanzibar


Meneja Miradi Maalumu wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Emma Oriyo akikabidhi kwa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi hundi ya Sh.milioni 10 zilizotolewa na kampuni hiyo kwa ajili ya kusaidia waathirika wa ajali ya Mv.Spice Islander. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Unguja.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi akimshukuru Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu baada ya kupokea mchango wa TBL, wa sh. mil. 10 za kusaidia waathirika wa ajali ya Mv.Spice Islander. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Unguja.Katikati ni Meneja Miradi Maalum wa TBL, Emma Oriyo.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi akisalimiana na Mwakilishi wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Zanzibar, Mweidady Mbaga baada ya kupokea mchango wa TBL, wa sh. mil. 10 za kusaidia waathirika wa ajali ya Mv.Spice Islander. Hafla hiyo ilifanyika mwishoni mwa wiki mjini Unguja.Kulia ni Meneja Miradi Maalum wa kampuni hiyo, Emma Oriyo na Ofisa Uhusiano wa kampuni hiyo, Dorris Malulu.

No comments:

Post a Comment